Monday, June 15, 2015

Azam TV yabadili habari, yaajiri watangazaji wapya !!!

Watangazaji wa Azam TV (kutoka kushoto) ni Raymond Nyamwihula, Zainab Chondo, Rehema Salum, Nurdin Suleiman, Fatuma Almasi Nyangasa, Baruani Muhuza, Ivona Kamuntu na Charles Hilary.

Kuanzia leo taarifa ya habari ya Azam TV itakuwa ikisomwa na watangazaji wawili na kutakuwa na pea tatu tofauti za watangazaji.Kuanzia leo taarifa ya habari ya Azam TV itakuwa ikisomwa na watangazaji wawili na kutakuwa na pea tatu tofauti za watangazaji.


Tido Mhando (Naibu Mtendaji Mkuu wa Azam Televisheni)

Naibu Mtendaji Mkuu wa Azam Televisheni, Tido Mhando alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa wamejiandaa vilivyo kuhakikisha kuwa mbali na studio bora wanakuwa pia na kikosi cha wanahabari wenye uwezo mkubwa.

“Hapana shaka tunao vijana wazuri sana, lakini pia tulihitaji waandishi wenye uwezo na ujuzi wa hali ya juu ili kuendana na mikakati, fikara na mipango yetu ya kufanya mageuzi makubwa ya hali ya juu ili kuendana na mikakati, fikara na mipango yetu ya kufanya mageuzi makubwa ya hali ya utangazaji wa habari za televisheni nchini,” alisema Tido.


Tido aliwataja baadhi ya waandishi na watangazaji ambao wameungana na Azam TV kuwa ni Charles Hilary, Baruani Muhuza, Ivona Kamuntu na Fatuma Almasi Nyangasa.

“Watangazaji hao sasa wataungana na wasomaji wetu wazuri wa siku nyingi Rehema Salum na Nurdin Suleiman kukamilisha pea tatu za wasomaji wa mtindo wa wawili wawili,” alifafanua Tido.
Tido alisema leo na kesho habari itasomwa na Charles Hillary na Ivona Kamuntu wakati siku mbili nyingine itakuwa ni zamu ya Baruhani Muhuza na Fatuma Nyangasa huku Rehema Salum na Nurdin Suleiman nao wakiwa na zamu yao.

Alisema licha ya taarifa ya habari ya saa mbili usiku pia wanatarajia hivi karibuni kuanzisha taarifa ya habari ya saa saba mchana itakayokuwa ikiendeshwa na Zainab Chondo na Raymond Nyamwihula.


“Mpango wote huu wa mabadiliko haya ya utangazaji na upatikanaji wa habari wa Azam TV utakuwa unasimamiwa na kuratibiwa na Joseph Warungu aliyekuwa Mwafrika wa kwanza kuongoza kitengo cha BBC cha Focus on Africa,” alisema Tido.


Source: Mwananchi

No comments:

Post a Comment